查看原文
其他

Habari Leo|中坦携手抗疫工作中的上外视角

SISU-TATAMA 上外东非研究中心 2023-01-01

      7月4日,上海外国语大学东非研究中心副主任、东方语学院斯瓦希里语专业教师宁艺在坦桑尼亚报纸《每日新闻》(Habari Leo)发表题为《中坦携手抗疫》(“China, Tanzania zilivyoungana kukabiliana na Covid-19”)的斯瓦希里语评论文章,系统介绍了中坦两国在防范新型冠状病毒肺炎疫情工作中精诚合作、共同抗疫的事实,有力驳斥了部分非洲媒体对中国抗疫工作与援非工作作出的片面论断。

       *《每日新闻》(Daily News)是坦桑尼亚国营新闻出版集团——标准报业 [Tanzania Standard (Newspapers) Limited] 旗下最重要的报纸品牌,分为英语版与斯瓦希里语版两个版本,“Habari Leo”是其斯瓦希里语版本。







中坦携手抗疫


       近日,坦桑尼亚主流报纸《公民报》发表了一篇名为《新冠肺炎疫情中的排外情绪与污名化令人震惊》的文章,文章中指出:“关于中国是新冠病毒的‘起源地’以及中国掩盖疫情真相的不实言论旨在破坏中非友好关系,削弱中国在非洲国家中的影响力。”

       由于新冠病毒最初在中国爆发,某些不怀好意的网络评论家声称,所有的中国人都是病毒携带者,这些言论造成了民众对中国人甚至亚裔群体的歧视和恐慌。更有甚者,认为非洲作为全球最不发达的地区,必将在此次疫情中首当其冲。事实上,这些落井下石的言论是部分政客为了转移国内抗疫不力的矛盾而故意寻找的话题与借口。

 

“病毒起源说”与“疫情瞒报说”

       尽管批评者们一再声称中国在疫情爆发初期故意隐瞒真实情况,根据世界卫生组织(WHO)公布的抗疫时间轴来看,早在一月初,中国就已公开分享了COVID-19的基因序列。与此同时,世卫组织在本组织三个层级(总部、区域总部和国家一级)组建事故管理支持小组,宣布进入抗疫紧急状态。根据世卫组织的预估,正是由于中国在第一时间对外公布了疫情相关信息,有效的阻止了数万民新冠病毒的新增感染者。著名期刊Science也曾在发文中公开表示:中国采取的紧急措施有效地控制了疫情的蔓延,为其他国家争取了宝贵的防疫时间。

       关于“病毒起源说”,尽管存在阴谋论认为病毒是由武汉国家生物安全实验室人为制造的,美国情报机构经过科学的考证证实新冠病毒是由自然进化而来的,并非人为制造。

 

中坦携手共渡难关

       早在疫情爆发初期,坦桑尼亚总统马古富力就曾向习近平主席致慰问信。马古富力在信中对中国政府采取的迅速有力措施及中国人民展现出的勇气和决心表示赞赏,认为这些措施有力地控制了疫情在全球范围内的蔓延。坦桑尼亚坚信,在习近平主席的坚强领导下,中国必将以坚韧不拔的精神,早日战胜这一全球共同威胁。坦方将坚定地同中方站在一起,共渡难关。

       现下坦桑与年初的中国遭遇着相同的情形,中国也将向坦桑尼亚民众不遗余力的伸出援手。到目前为止,中国政府已向桑给巴尔捐赠了第一批抗疫物资,包括2000个N95口罩、10000个医用外科口罩、2000件防护服、2000副护目镜、10000副手套、10000个鞋套和500个红外测温仪。马云基金会和阿里巴巴基金会已向坦捐赠包括呼吸机、检测试剂、口罩、防护服等在内的防疫物资。中国驻坦使馆和在坦中资企业也纷纷向坦方捐赠了医疗物资和用于修建隔离中心的建筑材料。

       此外,为了给非洲提供技术支持,中国外交部和国家卫健委已组织召开三次中非疫情防控专家视频会议,中坦专家在会议中交流了疫情防控和疾病治疗的知识与经验。中方将继续加强与非洲国家在公共卫生和疾病防控上的合作,携手共同战胜疫情。

 

关于捐赠物资质量低劣的不实言论

       有人声称中国捐赠的防疫物资质量低劣,并不能有效的起到防控作用。更有甚者怀疑捐赠口罩中也携带着新冠病毒,加剧了病毒的传播。

       事实上,中国捐赠的口罩等防疫物资都是严格按照ISO质量标准生产的。据悉此前捐赠的口罩、防护服等已经分发给一线医护人员投入使用,至今为止未曾出现任何质量问题。

       关于产生“质量低劣”的不实言论的原因。有些是因为不同国家间产品质量标准存在差异,例如欧洲国家使用的FFP1型口罩及中国使用的KN95型口罩,尽管型号不同,均能起到有效的防护作用。

       另有一些不怀好意的政客们企图通过污名化破坏中非关系,通过挑起外部争端转移本国因抗疫不力造成的恐慌与矛盾。

 

中国提供抗疫援助的动机

       关于中国协助非洲抗击疫情的动机,阴谋论者认为中国想借此机会加大对接受援助的非洲国家的控制,从而实现资源掠夺的目的。这一言论是非常荒诞的。因为中坦两国自古以来就有着相似的历史与相近的遭遇,两国间的友谊也是源远流长。当新冠病毒最早在中国爆发的时候,马古富力总统就曾在第一时间发出慰问,表示坦桑人民会支持中国实现抗疫成功。所以在疫情进一步蔓延的今天,中国也要投桃报李,向坦桑民众提供尽可能多的援助支持。

       作为第一个受到疫情冲击的国家,中国时刻准备着将成功的抗疫经验分享给其他有需要的国家。

 

中坦人民携手抗击疫情

       除了中方提供的抗疫援助外,我们还有数万名在坦华侨与坦桑民众携手共渡难关。

       尽管坦桑尼亚在疫情爆发初期就关闭了所有学校,达累斯萨拉姆大学孔子学院(CIUDSM)的老师们仍然在疫情期间坚持通过网络设备进行线上教学。张银风老师是达大孔院的一名志愿者老师,今年是她在孔院教授汉语的第二年。张老师说:“线上教学不但是为了帮助坦桑本地的学生持续学习汉语,更是为了帮助他们在困难时期树立信心。我们希望所有的学生们都能平平安安地度过疫情,因此除了线上教授汉语知识,我们还会普及一些防疫抗疫的常识和经验。”

       最后,疫情没有国界。新冠病毒是全人类面临的一个共同的灾难,在这场风波中没有一个国家可以幸免。因此我们更需要携手互助,共渡难关。相信在中国的帮助下,坦桑的疫情也能很快的得到控制。但愿坦桑民众早日战胜病毒,恢复以往的生机与活力。

作者|宁艺

单位|上海外国语大学


原文:


China, Tanzania zilivyoungana kukabiliana na Covid-19

 

Hivi karibuni gazeti moja la kila siku liliandika habari yenye lengo la kuvuruga uhusiano mzuri kati ya China na Afrika ikiituhumu kuwa chanjo dhidi ya virusi vya corona na kwamba, China ilichelewa kutoa habari za maambukizi ya mlipuko huo.

 

Ukiyatafakari kwa makini madai hayo, utabaini yanalenga kuharibu uhusiano mzuri uliopo kati ya Afrika na China na pia, kupunguza ushawishi wa China barani Afrika.

 

Lawama hizo zinazotokana na China kuwa nchi ya kwanza kukumbwa na mlipuko wa Covid-19 mwishoni mwa mwaka jana kabla ya kusambaa katika nchi nyingine duniani, haziingii akilini kutokana na ubaya wa lengo.

 

Mwandishi katika makala hiyo anawachukulia raia wa China kama chanzo cha virusi vya Corona hali inayoleta hofu na ubaguzi dhidi ya Wachina pamoja na Waasia popote walipo duniani.

 

Hoja ya mwandishi huyo haikuishia kuilaumu China na wananchi wake pekee, bali pia alizungumzia Bara la Afrika na kusema kwa kuwa halijaendelea kiteknolojia, litaathirika zaidi na mlipuko huo.

 

Maneno yote yaliyoandikwa ya kubeza uwezo wa nchi za Afrika kukabiliana na ugonjwa huo, ukiyaangalia utaona ni siasa yenye lengo la kusambaza uongo na kupunguza uwezo wa ndani kukabiliana na maambukizi hayo kwa kusababisha kutojiamini.

 

Madai ya kuficha ukweli

Ingawa kuna wachambuzi na wanasiasa wanaodai kwamba China imeficha ukweli kuhusu chanzo cha virusi vya Corona na kushindwa kuzuia maambukizi kuenea zaidi, ukweli ni kuwa China ilitimiza wajibu wake kwa kasi kubwa baada ya kubaini uwapo wa mlipuko huo.

 

Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Afya Duniani (WHO), China ilitoa taarifa kwa shirika hilo mapema mwanzoni mwa mwezi Januari 2020.

 

WHO ilichukua hatua za haraka na kuunda Tume maalumu ya kukabiliana na COVID-19 mara moja.

 

Taarifa za WHO zinaonesha kuwa, taarifa zilizotolewa na China kwa wakati zimesaidia kuzuia idadi kubwa ya watu kupata maambukizi.

 

Jarida la kitaaluma la Sayansi nalo lilikiri hatua za haraka za China kupunguza usambaaji wa virusi hivyo kwa nchi nyingine kutokana na kujikinga.

 

Kuhusu “chanzo cha virusi vya Corona”, ijapokuwa China imeshutumiwa kutengeneza virusi vya Corona katika maabara kwa kudhamiria, mkurugenzi wa Ofisi ya Intelejensia ya Marekani anasema wamechunguza kwa kina na kuungana na wanasayansi wengine kuwa chanzo cha ugonjwa huo ni cha kiasili, wala siyo kutengenezwa kwa dhamira.

 

Tanzania, China zilivyoungana katika vita dhidi ya Corona

Februari 3 mwaka huu, wakati maradhi ya COVID-19 yalipolipuka kwa nguvu nchini China, Rais wa Tanzania, John Magufuli alituma salamu za rambirambi kwa Rais Xi Jinping kuhusu janga hilo la kutishia.

 

Katika salamu zake, Rais Magufuli alisifu hatua za haraka na zenye nguvu zilizochukuliwa na Serikali ya China na ujasiri uliooneshwa na watu wa China.

 

Rais Magufuli alisema Tanzania itasimama pamoja na China ili kulishinda janga hilo kwa haraka.

 

Wakati nchi za Tanzania na China zikiwa zinakabiliwa na janga hilo la aina moja, China imetoa misaada kwa Tanzania bila kusita.

 

Hadi Mei 16 mwaka huu, China imetoa msaada wa vyombo vya kujikinga na virusi vya Corona kwa kila njia.

 

Kwa mfano, Serikali ya China imetoa vifaa tiba kwa Zanzibar zikiwemo barakoa 2,000 za aina ya KN95, barakoa 10,000 za upasuaji, nguo 2,000 za kujikinga dhidi ya virusi, jozi 10,000 za glavu, jozi 2,000 za miwani ya usalama, jozi 10,000 za vifuniko vya miguu, na vipimajoto 500 vya infrared.

 

Vifaa vya matibabu vilivyotolewa na Shirika la Mayun Foundations na Shirika la Alibaba Foundations ni pamoja na vitendanishi vya kupimia virusi, mashine za kupumulia, barakoa na glavu, nguo za kujikinga na kadhalika.

 

Zaidi ya hayo, Ubalozi wa China nchini Tanzania na kampuni za China nchini Tanzania pia zimetoa misaada mbalimbali, zikichangia vifaa vya matibabu na vifaa vya ujenzi vinavyotumika kujenga karantini za kujitenga. Michango hiyo imesaidia Tanzania kusuluhisha ukosefu wa vifaa tiba.

 

Licha ya hayo, ili kutoa misaada ya kidaktari na kiufundi, Wizara ya Mambo ya Nje ya China na Kamati ya Kitaifa ya Afya ya China ziliandaa mikutano mitatu kwa njia ya mtandao juu ya jinsi China ilivyodhibiti na kujikinga na maradhi ya COVID-19.

 

Katika mikutano hiyo, wataalamu wa China walishirikiana na maafisa wa Afrika juu ya namna ya kuzuia virusi na matibabu ya ugonjwa. China itaendelea kuwapa Waafrika uzoefu na misaada ya kupambana na maradhi ya Corona.

 

Ubora wa vifaatiba

Vifaa vilivyotolewa na Serikali ya China vyote vimezalishwa kwa kufuata kanuni za utengenezaji na vimekidhi viwango vya ubora wa kimataifa.

 

Vifaa kama barakoa na nguo za kujikinga vimesambazwa kwa madaktari na wauguzi wa hospitali nchini Tanzania na kufikia sasa, hakuna mtu yeyote aliyelalamika juu ya uhafifu wa vifaa vilivyotolewa na China.

 

Visa vilivyosababisha madai hayo ya “uhafifu wa vifaa” ni pamoja na viwango tofauti vya ukaguzi wa Shirika la Ubora wa Viwango Duniani (ISO).

 

Kwa mfano, watu wa nchi za Ulaya wanatumia barakoa za FFP1 huku watu wa China wanatumia barakoa za KN95, ingawa barakoa hizo ni za aina tofauti, zote zinaweza kuzuia virusi vya Corona kwa ufanisi mkubwa.

 

Misaada kwa nchi za Afrika

Watu wengine wametoa hoja kwamba China inazisaidia nchi za Afrika maana inataka kunyang'anya maliasili za Afrika. Hii siyo kweli.

 

China ilijenga uhusiano wa kirafiki na nchi nyingi za Afrika tangu zilipojipatia uhuru. Uhusiano na ushirikiano baina ya nchi hizi unaendelea vizuri mpaka leo.

 

Tanzania na China ni kama hivyo, zina historia za aina moja, tena zina urafiki wa tangu zamani sana. Wakati maradhi ya COVID-19 yalipolipuka nchini China, viongozi wa Tanzania pia waliitumia China salamu za pole na rambirambi.

 

Wakati wote pande hizo mbili zinasaidiana na kuungana mkono katika jukwaa la kimataifa. Hivyo ni lazima China irudishe hisani na misaada Tanzania inapokabiliwa na shida.

 

Kwa sababu China ni nchi ya kwanza kukumbwa na janga la Corona, Wachina wanahurumia sana nchi nyingine zinazokabiliwa na tatizo hili.

 

Sasa virusi vya Corona vimedhibitiwa kwa ufanisi mkubwa nchini China, hivyo Serikali ya China iko tayari kubadilishana uzoefu na nchi nyingine zinazohitaji misaada.

 

Kuishinda Corona

Zaidi ya misaada inayotolewa na China, nchini Tanzania kuna Wachina wengi wanaoishi nao wote wanashirikiana na Watanzania ili kuishinda Corona kwa haraka.

 

Ingawa shule na vyuo nchini Tanzania vilifungwa na kufunguliwa siku za karibuni kwa sababu ya ugonjwa, walimu wa Taasisi ya Confucius ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (CIUDSM) waliendelea kufundisha lugha ya Kichina kwa wanafunzi kwa njia ya mtandao.

 

Mwalimu Zhang Yinfeng ni mmojawapo wa walimu wa kujitolea katika CIUDSM. Huu ni mwaka wake wa pili kufundisha Kichina hapa Tanzania.

 

Anaseme kwamba,“Tunafundisha lugha ya Kichina wakati huu wa Corona si kwa lengo la kujifunza lugha tu, bali pia tunawapa wanafunzi moyo ili kuishinda Corona kwa haraka.”

 

“Tunatumaini wanafunzi wote wako salama katika kipindi hiki kigumu. Hivyo wakati tunapowafundisha ujuzi wa Kichina, pia tunawaambia namna ya kujikinga na ugonjwa.”

Mwandishi | Ning Yi , Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Taaluma za Kimataifa cha Shanghai




您可能也对以下帖子感兴趣

文章有问题?点此查看未经处理的缓存